Monday, 16 September 2013

KAMA ULIKUWA HUJUI,BASI HIKI NDICHO WCB TULICHOKIFANYA FIESTA MOROGORO USIKU WA JANA




Msimu wa Fiesta 2013,unaendelea na jana ilikuwa ni zamu ya
 watu wa Morogoro kupewa burudani harisi kutoka kwa watoto wa kitanzania,mimi na Crew yangu ya WCB tuliwasili Morogoro mapema mchana na kuungana 
na wasanii wenzangu,waliokuwa wameshatangulia.Kiukweli sitochoka
 kuwashukuru mashabiki wangu wa Moro kwa sapoti na mapenzi makubwa
 waliyoyaonyesha on stage,hawakuniangusha
 na hii inazidi kunipa deni la kuaandaa mambo mapya na mazuri zaidi kwa ajili yenu ..nisiongee sana,nakuachia picha ziongee zenyewe!!!

Baada ya kuwasili eneo la tukio,nikisalimiana na baadhi ya wasanii waliokuwa wametangulia..
mmh Recho kunitoleaa macho!!Linah anachekelea tu kwa mbali

Rommy Jones na Shadee wa Clouds

My boy Qboy msafi akifuatilia kitu kwa makini

Kwanza tukaanza kuwalewesha kwanza kama hivi..........



Hilo nyomi sasa..watu wangu wa Moro mlitisha saaana!!!





Ama nini...!!


Hapa ni mwendo wa kuimba wote tu



My boy Dummy

Rommy J on one&two


Noma sana...







Nikiitazama moja ya siraha yangu ya WCB,Imma pltnumz anavyowatendea haki mashabiki

Tulia bwana mdogo hebu nitizame mimi kwanza


Dummy







Ikafika ile time ya kumkalisha huyu bitozi wa Manzese




Brothermen vipi bado unabisha??

Ubaya  wenu wengi kayumba,elimu mliitupa sandakalawe!!!!

Dada zetu wanavaaga nguo za hivi kweli??huyu Nay vipi!!!


Bora nikimbie usije nipiga mbata..ha ah ah a..was so fun




Twangala Dozen &Fetty 


They call him Kiroboto the legendally,alikuwepo pia

Monday, 9 September 2013

GAREHT BALE ABURUZWA VIBAYA NA MESUT OZIL KATIKA MAUZO YA JEZI



Ozil ArsenalOzil Arsenal
Gareth Bale anaweza kuendelea kupokea maneno yasiyo ridhisha kwa kumbadili  Mesut Ozil katika klabu ya Real Madrid baada ya wauzaji wakubwa wa jezi za soka mtandaoni UKSoccershop.com kuthibitisha kwamba mauzo ya jezi za nyota mpya wa Arsenal yameyazidi yale ya Bale kwa kiwango kikubwa.

Madrid tayari wamekuwa katika hali ngumukwa kumruhusu Ozil kuondoka kwa ada ya uhamisho ambayo walilipa kwa Bale - hivyo kumfanya mchezaji huyo wa Wales kuwa mchezaji ghali zaidi duniani kwa ada ya uhamisho wa £86million.

Presha kubwa sasa ipo kwa Bale kuelekea mchezo wake wa kwanza na Real Madrid wikiendi ijayo, huku sasa namba za mauzo ya jezi zikionyesha kwamba ni mchezaji aliyembadili ndani ya kikosi cha Carlo Ancelotti ambaye ameshika usukani kwa kuuza jezi nyingi. 


Mkurugenzi wa UKSoccershop.com Simon Pretswell alisema: 'Ukiachana na masuala ya uwanjani, sehemu kubwa ya uhamisho ghali duniani huwa umetaliwa na sababu za kibiashara zinazokuja na ukubwa wa mchezaji husika.'
'Katika kesi ya Cristiano Ronaldo, Lionel Messi na mastaa wengine wa zamani kama David Beckham, hawa walileta fedha nyingi kwa klabu kwa mauzo ya jezi kupanda kwa kiasi kikubwa.'

Gareth Bale ameshindwa kuleta mauzo makubwa ya jezi kama ilivyo kwa Mesut Ozil na Neymar walipohamia kwenye vilabu vyao vipya katika dirisha hili la usajili.' 
'Kipaji cha Bale hakina mashaka, lakini hajawahi kuwa mmoja ya wauzaji wakubwa wa jezi katika premier league, huku mashabiki wakivutiwa zaidi na jezi za Wayne Rooney, Robin van Persie, Steven Gerrard na even Fernando Torres.'

Jack Wolper awataka wasanii wa kike WAJIHESHIMU kwa kutovaa mavazi ya nusu UCHI


.


Muigizaji wa filamu za  kibongo  maarufu  kwa  jina  Jackline Wolper amewaasa waigizaji wenzake wa kike kuacha kuvaa nguo za nusu uchi kwani ni kinyume na mila na tamaduni za kitanzania .

Wolper aliyasema hayo kufuatia kupigiwa kura na kushinda kama muigizaji wa kike mwenye muonekano wa kistaa...

Akizungumza katika kipindi cha filamu cha Take One kinachorushwa Clouds Tv , Wolper alisemakuwa  yeye hawezi kuvaa mavazi ya nusu uchi ila anavaa  mavazi yanayomsitiri mwili wake na bado anapendeza kuliko hao wanaovaa nusu uchi halafu hawapendezi.

"Nawashukuru  sana mashabiki wangu kwa kunipigia kura hadi kuibuka mshindi, na ni kweli najiamini kwa kuwa mimi hata siku moja huwezi kuniona nimevaa nguo za nusu uchi kama wengine" Wolper

IFUATAYO NDIYO LIST YA MASTAA 10 WANAOLIPWA MSHIKO MREFU HOLLYWOOD



Kwa mujibu wa Jarida na kampuni inayojishugulika na maswala
ya utafiti wa kuangalia maendeleo
na vipato vya wasanii,waigizaji na watu maarufu dunia,FORBES,hii ndio list
ya wacheza filamu nchini Marekani toka Hollywood
wanaoongoza kuwa na mshiko
mrefu zaidi Duniani.......



NIMEKUPANGIA LIST HII KWA MAJINA NA PESA WANAZOINGIZA:

1:Robert Downey Jr-IRON MAN (75 million$)

2:Channing Tattun-MAGIC MIKE,WHITE HOUSE DOWN(60 million$)

3:Hugh Jackmann-LES MISARABLE,XMAN(55 million$)

4:Mark Walhberg-TED(52 million$)

5:Dwayne 'The Rock' Johnson-Fast & Furious(42 million$)

6:Leonardo DiCaprio-Great Gatsby(39 million$)

7:Adam Sandler-Hotel Transylvania(37 million$)

8:Tom Cruise-Jack Reacher(35 million$)

9:Denzel Washington-Flight(33 million$)

10:Liam Neeson-Taken 2,The Grey(32 million$)

Friday, 30 August 2013

MTAZAME DIAMOND AKITAMBULISHA VIDEO YA MY NUMBER ONE ILIVYO HAPPEN NDANI YA SERENA HOTEL



Napenda kutoa Shukrani zangu za dhati kwa
Mwenyezi Mungu kwa kuweza kunifanikisha
hadi kufikia hapa muda na wakati kama huu...
Usiku wa tarehe 29.08.2013 nilikuwa na Launch
video yangu inayotambulika kama
My Number One,nilianda tafrija fupi kwenye
 hoteli ya nyota tano,Serena Hotel jijini Dar Es Salaam


,ili kuweza kujumuika
na ndugu,jamaa na marafiki wa karibu kuwonesha
kile kitu ambacho nimetumia muda mwingi
kutengeneza,kabla ya kuiachia nikaona vyema
waipitie kabla mtu wangu wa kweli ujaicheki.


Shukrani zangu nyingie ziwaende kwa wageni waalikwa 
wote kufika na kutoa support na kushow love kwangu
Sina cha kuwalipa bali kusema asante na mzidi kutegemea
kazi nzuri toka kwangu...

Napenda kuwashukur wasanii wenzangu waliofika
kuangalia video yangu na kuzishukur media zote
na Blogs zote zilizofika kuakikisha wakipata
matukio muhimu kabisa.

Mtu wangu wa kweli unaweza ukache Exclusive Photo kwaajili yako
ujione kilichojiri usiku wa My Number One video Launching 
Serena Hotel.

WASAFI......WCB

Picha Picha tu zinahusika sehemu kama hizi.....Kumbukumbu tosha.


William Malecella or U can Call Him Lemutuz.....

I-view Media C.E.O & Founder Raqeey wa kulia na Mpenzi wa Nancy Sumari.
Nancy Sumari,Kulia akiteta jambo na mgeni
mwingeni mwalikwa....Sehemu kama hizi
ukutanisha watu na kubadilishana mawazo...

Kutoka Kushoto A.Y,Shaa,Bench Mark Founder
 & EBSS Chief Judge Madam Rita & Salama Jabir
ndani ya nyumba....





Kila mtu Busy na simu kuangalia kianchojiri
kwenye upande wa pili wakisubiria Launching ya
My Number One...




Uncle Salu akukosekana nae,kuhakikisha mambo yanaenda sawa
pembeni ni mama yangu Mzazi BI Sandrah....



Mama Yangu kipenzi akukosekana,Asante
sana mama kwa kufika,Binafsi nafarijika
kuona hata mama yangu mzazi anakubali kazi zangu...

Kelvin Twisa toka Airtel nae ndani ya Jumba....






Hizi unazoona kwenye Screen ndani ya picha
ni baadhi ya Clip za Behind the scene ya
My Number One....



Babu tale toka Tip Top Connection & Fella toka TMK...
Toka Bongo MOVIE JAY B & RAY walikuwepo kuona
 kile ndugu yao wa karibu nini nafanya...





Madee toka Tip Top Connection nae alikuwepo...

Proffesor Jay nae alikuwepo kuakikisha anashuudia
 kile ambacho alikuwa akikisikia...





Abdallah au waeza muita Mjukuu wa Ambua basi tumuite Dullah Planet Bongo
ndiye alikuwa anaongoza gurudumu ili kuanzia mwanzo hadi mwisho...

Wenzetu wanaita Master Of Ceremony but
binafsi watu wanaoendesha shuguli yoyote
ya maongezi au Sherehe namuiaga msema Chochote....



Nikitokeza kwa Stage kusalimiana na wageni wangu waalikwa waliofika kwaajili
yangu kushuudia uzinduzi wa Video yangu Mpya.....


Hahaha usiombe usikie nilichoambiwa
 hapa mbele....Lazima utatabasamu...




Mama yangu akitabasamu kuonesha ishara ya furaha ndani yake...


Furaha ilioje.....imezidi mpaka imepitiliza...uwiiii
mama yangu nakupenda sana...

SENEDA vipi tena....? Macho Kodoo wapi....

Muda baada ya wadau wangu na watu
wangu wa karibu kuiona video hiyo
hii ilikuwa zawadi yangu kwao,kwa mara ya
kwanza nimetumbuiza my number one
kwenye stage....

Gentleman's.......
Taratibu......
Aghaaa.....Tatu kidonda chako kwangu maradhi......
Kwa mahaba uliyonipa...Nimenogewa.....
Ajajaja Mizuka imepanda....

Woshhhhh.....Balaa sana...... 










Baada ya kutumbuiza nilikuwa na machache ya kuzungumza nao....




Kutoka Kushoto Sheddy Clever Producer aliefanya My Number one.....



Ommy Dimpoz...Tupogo nae alikuwepogo ndani ya Nyumba.....







G5 CLICK.....

Nikikumbatiana na Ommy Dimpoz...Thanks Man kwa kutokea...





Nilikuwa Busy sana toka nimewasili baada ya
 kila kitu ilikuwa time ya kuzunguka na kuongea na kusalimu
wageni waalikwa......Mmoja wapo Kaka yangu
Dully nilienda kusalimiana nae kitambo atujasomana...

Ukikaa na huyu mtu kamwe uwezi nuna pasipo sababu ya msingi.....
Qboy Msafi...Assistance wangu wa karibu...







Nikisikiliza jambo la muhimu toka kwa
 Meneja mahusiano wa Airtel Tanzania...


Dude a.k.a Yahya au waeza mwita Bongo
Dar Es Salaam alikuwepo pia....

Nelly toka G5 Clik ya Clouds Media Group nae ndani...
Ommy Dimpoz & Qboy msafiii
My Blood Rommy Jones au waweza muita Vice
President wa wasafi,Ommy Tupogo,Qboy & Prince Dully

Family....Romeo & Mwengi Ali shem lake....
My Fresh n Blood Sister ESMA KHAN nae
 akukosekana licha ya kuwa mbali kidogo lakini
aliweza wahi kuja kunipa support mdogo wake...

Kulikoni Romeo wamfokea Penniel........??? Sielewi
Esma Khan & True Boy Nay....

Kichwa mimi hapa,SALMA msangi & Proffesor J....
Essy & I



Mechoka sana muda huo ilinibidi k
ukimbia kurudi hotelini kupumzika
baada ya siku 4 nyuma kuwa resi muda mwingi
kufanikisha jambo ili,Namshukuru
sana Mungu kwa kufanikisha Jambo ili na Crew
 Yangu nzima ya WASAFI CLASSIC BEIBY

Doooh......Noma sana

Memaliza watu wang wa kweli.........